agnesshija2005@yahoo.comWAMO KIMBISA, DK MASSABURI NA IDD SIMBA, RIPOTI YAKE KUTOKA KARIBUNI
Patricia Kimelemeta
SAKATA la uuzaji wa Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA), limezidi kupamba moto baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Ludovick Utouh, kuwataja vigogo wapya waliohojiwa na shirika lake kutokana na kutajwa kwamba walishiriki katika mchakato wa uuzaji wa hisa za shirika hilo.Akizungumza na Mwananchi jana, Utouh aliwataja vigogo hao ambao alisema baadhi wameshahojiwa kuwa ni Mwenyekiti wa Bodi, Idd Simba na Mkurugenzi wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena.
Vigogo wengine ambao Utouh alisema wanatarajiwa kuhojiwa wakati wowote ni Meya wa jiji la Dar es Salaam Dk Didas Masaburi na mtangulizi wake, Adam Kimbisa pamoja na Meneja Mkuu wa UDA, Victor Milanzi.
“Sisi hatufanyi kazi kisiasa, tunafuata sheria na taratibu zote zinazotakiwa katika kufuatilia suala hilo. Hivyo basi, lazima tuwe makini kwa kujiridhisha na taarifa inayotolewa," alisema CAG.
Utouh alisema ili ripoti hiyo iweze kukamilika na kuondoa hofu ya kumwonea mtu, wahusika wote waliotajwa kwenye sakata hilo wanapaswa kuhojiwa.
Agosti 13 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi) Keptein mstaafu George Mkuchika, alitekeleza agizo la waziri mkuu na kumpa CAG barua ya kufanya ukaguzi wa UDA ndani ya mwezi, lakini sasa ni zaidi ya miezi minne matokeo hayajatoka.
Hata hivyo, CAG Utouh akizungumzia sababu za kuchelewa kwa uchunguzi huo aliema; “Tulitaka kutoa nafasi kwa watuhumiwa kupata fursa ya kujitetea."
Utouh alifafanua kwamba, lengo hilo la kutenda haki ndilo lililofanya ofisi yake kuwahoji wahusika wote waliotajwa kushiriki kwenye mchakato huo ili ripoti itakayotoka isiwe ya kumwonea mtu.
Aliongeza kwamba kutokana na hali hiyo, wanaamini kuwa kukamilika kwa ripoti hiyo, kutaisaidia serikali kutoa uamuzi sahihi kuhusu sakata hilo na kuwaachia wale ambao wanaweza kuingizwa kwa makusudi kutokana na tofauti zao za kisiasa.
Utouh alifafanua kwamba, hadi jana Kampuni ya KPMG iliyopewa jukumu la kufanya ukaguzi huo, ilikuwa ikikamilisha ripoti yake ambayo, wanaamini inaweza kutolewa mwishoni mwa mwezi huu na kuikabidhi serikalini kwa ajili ya hatua zaidi.
Sakata lilivyokuwa
Serikali ilibaini kuwepo kwa ukiukwaji wa kisheria katika uuzaji wa UDA Agosti mwaka jana, jambo ambalo lilisababisha kuundwa kwa tume ya uchunguzi.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliagiza kuunda tume ya kuchunguza sakata hilo huku akizitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na CAG, kuchunguza mchakato mzima wa uuzaji wa hisa za shirika hilo kwa kampuni hiyo ya Simon Group Limited.
Habari ambazo Mwananchi limezipata zinadai kuwa tayari Takukuru pia walishawahoji baadhi ya watu kuhusu suala hilo.
UDA lilikuwa linamilikiwa kwa pamoja kati ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Serikali Kuu, kupitia Hazina, wakiwa na jumla ya hisa milioni 15, kila hisa moja ikiwa na thamani ya Sh 100.
Mchanganuo wa hisa za UDA unaonyesha kuwa, halmashauri ya jiji la Dares Salaam ilikuwa inamiliki asilimia 51 na Hazina asilimia 49 za hisa hizo.
Hata hivyo, Februari 11 mwaka jana, bodi ya wakurugenzi ya UDA, chini ya Idd Simba, ilikutana na uongozi wa Simon Group ikiongozwa na Kisena na kusaini mkataba, ambao ulithibitisha kwamba UDA ilikuwa imeiuzia Simon hisa milioni 7.8 sawa na asilimia 52.6 ya hisa zote kwa thamani ya Sh bilioni 1.142.
Kwa mkataba huo, Simon Group ingekuwa mwanahisa mkubwa katika umiliki wa UDA kwa vile Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na Hazina, wangebaki na hisa milioni 7.7, ambazo ni sawa na asilimia 47.4.
Baada ya mkataba kusainiwa, kipengele cha kwanza kiliitaka Simon Group kulipa asilimia 25 ya fedha za ununuzi wa hisa za UDA , ambazo kati ya fedha jumla Sh bilioni 1.142, ni sawa na kutanguliza Sh 285.6milioni.
Fedha hizo zilipaswa kulipwa ndani ya siku 14, tangu kusainiwa mkataba huo ili kuufanya utambulike kisheria na ndipo, Simon Group ililipa fedha hizo siku hiyo hiyo.
Ndani ya Bunge
Uuzwaji wa UDA ulitikisa Mkutano wa nne wa bunge baada ya wabunge kutaka hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahusika, huku wabunge wa mkoa wa Dares Salaam wakijikuta katika malumbano na Dk Masaburi.
Wakati mvutano huo ukiendelea, wamiliki wa Simon Group Ltd, walijitokeza hadharani na kuwaambia waandishi wa habari kwamba umiliki wake umekidhi vigezo vyote katika kumiliki Hisa ndani ya UDA.
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Simon Group, Robert Kisena alisema kampuni yake ilifuata vigezo vyote vilivyotakiwa na kwamba imejizatiti kuliendesha Uda bila wasiwasi na kwamba hadi wakati huo walikwishawekeza kiasi cha Sh760 milioni.
Hata hivyo, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) kupitia kwa Mwenyekiti wake, Zitto Kabwe nayo ilisema kuwa mkataba huo ni batili kutokana na fedha zilizonunua hisa husika kuwekwa kwenye akaunti ya kada wa Chama Cha Mapinduzi na mwanasiasa wa siku nyingi, Iddi Simba.
“Taratibu hazikufuatwa,na uamuzi wowote utakaofanyika ni batili kwa kuwa tayari sisi tumeshaanza mchakato wa kubaini kilichopo ndani ya mkataba huo ikiwa ni pamoja kumuagiza CAG na tayari Spika ana taarifa hizo,’’alisema Zitto.
picha zetu (display)
this blog has no limits its designed to put good photos of u
Jan 11, 2012
Poshooo
Mwezi Disemba mwaka 2011 Waziri wa Fedha na Uchumi alimwandikia barua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) kumwahidi mambo yepi Serikali ya Tanzania itafanya ili kurekebisha Bajeti yake. Utaratibu huu hufanyika kila mwaka kupitia mpango unaoitwa ‘Policy Support Instrument (PSI). Katika barua hiyo Waziri wa Fedha wa Tanzania ameahidi kwamba Serikali itafanya juhudi kupunguza matumizi ili kuweza kupunguza uwiano wa nakisi ya Bajeti na Pato la Taifa (fiscal deficit to GDP ratio) kutoka asilimia 7.2 mpaka asilimia 6.6 ya Pato la Taifa.
Waziri wa Fedha na Uchumi ameiambia IMF kwamba ifikapo mwisho wa Mwezi Disemba mwaka 2011 (wiki mbili zilizopita) Baraza la Mawaziri la Tanzania limefikia maamuzi ya kupunguza nakisi ya Bajeti kwa kiwango kilichotajwa. Maeneo yanayotajwa ni Pamoja na Miradi ya Maendeleo ambapo jumla ya miradi yenye thamani ya Tshs 157bn itakatwa. Waziri
wa Fedha ametaja miradi hiyo katika Ukarabati na Ujenzi wa Miundombinu.
wa Fedha ametaja miradi hiyo katika Ukarabati na Ujenzi wa Miundombinu.
Kambi ya Upinzani Bungeni inapinga kuondolewa kwa miradi ya maendeleo ili kupunguza matumizi ya Serikali. Kimsingi wakati kama huu ambapo hali ya uchumi ni mbaya na vijana wengi vijijini na mijini hawana ajira tunasisitiza umuhimu wa kutumia zaidi kwenye miradi ya maendeleo.
Punguza matumizi ya kawaida
Kambi ya Upinzani Bungeni inarejea wito wake kwa Serikali kupunguza matumizi ya kawaida ili kupata fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo. Haiwezekani kamwe tukawa Taifa huru iwapo miradi yetu yote ya maendeleo inafadhiliwa na wahisani. Kiwango kidogo tulichokiweka katika Bajeti ya mwaka huu ndicho hicho sasa kinakatwa na hivyo miradi yote ya maendeleo kubakia kwa wahisani ama kwa mikopo au misaada. Kiwango cha Tshs 203bn sawa na 0.5% ya Pato la Taifa ambacho Serikali imeahidi kupunguza ni kidogo mno na kinalenga kuumiza watumishi wa kada ya chini ya Serikali na sio viongozi wakubwa. Bajeti ya Mafunzo inayoenda kukatwa itaumiza Manesi na Walimu au watumishi wanaoongeza ujuzi ili kuboresha kazi zao. Serikali ikate matumizi yote yasiyo ya lazima na hasa posho (360bn), ipunguze matumizi ya magari na yale yasiyo na uhitaji yapigwe mnada na viongozi wote isipokuwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika na Jaji Mkuu washushwe madaraja ya kusafiria kwenye ndege. Safari zote ambazo hazina mahusiano na miradi ya maendeleo zipigwe marufuku kwa muda wote wa miezi sita ya Bajeti iliyobakia.
Serikali ihakikishe matumizi katika Sekta ya Elimu na Afya hayakatwi kabisa ili kuhakikisha tunalinda mafanikio kiduchu ya upanuzi wa sekta hizi na kuongeza uwezo wa Serikali kutoa huduma bora kwa wananchi hasa wa vijijini.
Matumizi ya Maendeleo yasiguswe, yaongezwe
Tayari imeonekana kwamba katika kipindi chote cha nusu ya Bajeti Halmashauri za Wilaya hazijapata fedha za maendeleo. Mfano Halmashauri ya Wilaya Kigoma imepata asilimia 0.3 tu ya Bajeti ya Maendeleo ilhali Halmashauri ya Mji wa Mpanda imepata asilimia 4 tu. Ni dhahiri miradi ya maendeleo kwa maeneo mengi ya vijijini itakwama kwani ni wazi kabisa kwamba Halmashauri hazipati fedha zote za Bajeti ya Maendeleo. Serikali itambue kwamba miradi ya maendeleo sio anasa bali ndio vyanzo vya baadaye vya mapato ya serikali. Miradi ya maendeleo hutoa ajira kwa wananchi na hivyo kuwapunguzia umasikini wa kipato. Jumla ya Tshs 157bn zinazotakiwa kukatwa zisikatwe bali ziongezwe ili kupata fedha za kurekebisha miundombinu kama Reli ya Kati.Kwa mfano Reli ya Kati inahitaji Tshs 200bn katika kipindi cha miaka 3 ili iweze kusafirisha mizigo tani 1.5m kwa mwaka kila siku na kuzalisha faida.
Ongeza Mapato ya Ndani
Inashangaza kwamba katika mpango wa Serikali kupunguza nakisi ya Bajeti mkazo umewekwa kwenye kuondoa miradi ya maendeleo badala ya kuongeza mapato. Nakisi hupunguzwa ama kwa kupunguza matumizi au kwa kuongeza Mapato. Serikali katika Taarifa yake kwa IMF imeibua njia moja tu ya kuongeza mapato, kodi ya mapato kutoka Kampuni ya Geita Goldmine. Huu ni uvivu wa kufikiri.
Serikali imeambiwa mara kadhaa suala la kuanza kutumika kwa sheria mpya ya madini kwa Kampuni za Madini zilizokuwapo. Makusanyo ya Mrahaba peke yake kwa sheria mpya, kiwango kipya na kanuni mpya ya kukokotoa ingeongeza mrahaba mpaka Tshs 203bn kutoka Tshs 99bn za sasa. Kwanini Serikali ianvuta miguu katika kutekeleza hili? Waziri wa Nishati na Madini aliahidi Bungeni kwamba mazungumzo na Kampuni za Madini yanaisha Mwezi Septemba. Mbona Serikali imekuwa BUBU katika hili?
Serikali iliahidi kuangalia suala la mauzo ya mali za makampuni zilizoko Tanzania na kodi ambayo tunapaswa kukusanya, Serikali imekuwa kimya kabisa katika suala hili. Marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa kuondoa msamaha kwenye ‘deemed capital goods yangeongeza mapato ya Serikali kwa kiwango kikubwa na kupunguza mzigo wa
misamaha ya Kodi.
misamaha ya Kodi.
Uwajibikaji kwa Bunge
Inashangaza zaidi kwamba sasa imekuwa ni mtindo kwa Serikali kutoa ‘commitments’ muhimu za kibajeti kwa Shirika la IMF badala ya wananchi kupitia Bunge. Bunge limepitisha Bajeti, mapitio yeyote ya Bajeti yanapaswa kuidhinishwa na Bunge. Bila kufanya hivyo maana ya Bunge kupitisha Bajeti inakuwa haina mantiki na uhuru wa Taifa letu unakuwa haupo kwetu.
Umuhimu wa Bunge kutunga haraka Sheria ya Ofisi ya Bajeti ya Bunge (Parliamentary Budget Act) sasa unaonekana waziwazi. Muswada umewasilishwa Bungeni na Wabunge binafsi kutaka kuundwa kwa mfumo wa kuisimamia Serikali katika Bajeti. Ofisi ya Spika wa Bunge ihakikishe muswada huu unachapishwa katika Gazeti la Serikali mara moja ili usomwe kwa mara ya kwanza katika mkutano wa Sita wa Bunge na kutungwa kuwa sheria katika mkutano wa Saba.
Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ilete mpango wa kupunguza matumizi Bungeni ili ujadiliwe na kuidhinishwa na Bunge kabla ya kuanza kutumika. Vinginevyo Mpango wa Serikali kwa IMF utakuwa ni kudharau wananchi na kuuza uhuru wetu kwa Shirika la Fedha la Kimataifa. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema mwishoni mwa miaka ya Sabini ‘toka lini Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limekuwa Wizara ya Fedha ya Kimataifa (International Ministry of Finance)?’
Kabwe Zuberi Zitto, Mb
Waziri Kivuli Fedha na Uchumi
Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni (NKUB)
Dar es Salaam, 10 Januari 2012.
breaking news the death of Mzee Kipara
With the success of twenty to thirty something artists in Tanzania, it is easy to forget that even before Bongo Flava or YouTube and, even the Internet for that matter – Mzee Kipara was there. When we went to film Bongoland II in Dar, the casting director – Gervas Kasiga told me that he found a perfect old man to play the imam in the movie. He then said – once you hear his voice you will know who he is. And, sure enough, once I heard him I recognized his voice immediately. Mzee Kipara is a veteran actor who worked for Radio Tanzania for many years. He was part of the talented cast that was heard weekly in thrilling radio drama productions.
As a kid growing up in Bukoba, the radio reception was never clear, and so sometimes all we could hear were pieces of an argument between two characters and the unmistakable deep voice of Mzee Kipara in most cases playing an elder, a teacher, or a grandfather.
Read more: MZEE KIPARA-TANZANIA’S ACTING ICON - BongoCelebrity agnesshija2005@yahoo.com
Jan 5, 2012
2012 is there any difference?
Tumaini University students study outside their classes due to lack of classrooms.
It was in 2009 whereby the student were promised good condusive classrooms for their studies,but its been three years now they are about to finish their school with no any promise made been fullfilled, though this is one of the University were by the students pay lots of money but yet is also one of the poor university that has no good environment for the students to learn.
one of the student said that "the university does not care on what condition are their students are in and they dont mind if their have the facility enough to facilitate us, because its been like this ever since the foundation of the University here in Dar es salaam and no changes have been seen to improve".
Hali halisi ndo hii.
Does this mean the Management dont Care? or They dont know?
Subscribe to:
Posts (Atom)